Ni muhimu serikali kushikana na vijana kusongesha SDGs: Vivian Joseph
Umoja wa Mataifa umekuwa ukipigia upatu vijana kujitokeza na kushiriki katika kusongesha ajenda ya maendeleo endelevu SDGs sasa ikiwa imesalia chini ya miaka 6 kabla ya kufikia ukomo mwaka 2030. Vijana katika sehemu mbalimbali duniani wanakumbatia wito huo kwa kushiriki kwenye miradi mbalimbali.